Breaking News

LHRC chawakutanisha Wadau Kutathimini Miaka 30 ya Demokrasia Tanzania

Wadau mbalimbali wakishiriki katika Mjadala katika Maadhimisho ya Siku ya Demokrasia Duniani ulioandaliwa na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC).


Na Hussein Ndubikile, Dar es Salaam
 

KATIKA kuadhimisha Siku ya Demokrasia Duniani, Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kimewakutanisha wadau kutathmini Miaka 30 ya Demokrasia tangu kuanzishwa kwa Vyama Vingi vya Siasa nchini mwaka 1992.

Akizungumza katika mjadala huo uliofanyika jijini Dar es Salaam Kaimu Mkurugenzi wa LHRC Felista Mauya amesema kuwa LHRC ni mdau na mtetezi mkubwa wa haki za binadamu.

“Kuadhimisha siku hii ni kuendeleza jitihada za kukuza na kulinda haki za binadamu,” amesema Felista.

Felista ameeleza kwamba Demokrasia ni kielelezo tosha cha ustawi wa haki za binadamu, pia ni ishara ya kuendeleza utamaduni wa ustaarabu na utii wa Sheria. Kwamba uwepo wa Demokrasia ni kiashiria cha utekelezaji wa dhana ya ushiriki na ushirikishwaji wa wananchi katika kufanya maamuzi ya kuchaguaviongozi wao.

Dkt. Bujari ameendeelea kueleza kuwa ili kufikia malengo ya kutokomeza maradhi ya Kifua Kikuu na UKIMWI, kwa miaka mitatu ijayo, zinahitajika Dola za kimarekani bilioni 130.2 na Global Fund pekee yake inahitaji dola za kimarekani bilioni 18.

Kwamba fedha hizo zitachangia kuendeleza mapambano ya kutokomeza maradhi hayo kwa kujenga ustahamilivu na mifumo ya endelevu ya afya na kuimarisha utayari katika kukabiliana na maradhi, hasa katika nchi zinazoendelea kama Tanzania ambapo hiyo itasaidia kufikia watu milioni 20 ifikapo mwaka 2026.

Amesema katika Sekta ya Afya kwa Tanzania pekee, mfuko huo umeweza kuchangia kiasi cha Dola za kimarekani bilioni 2.6 toka mwaka 2002 ambapo fedha hizo zimesaidia kupambana na magonjwa ya UKIMWI, Kifua Kikuu na Malaria.

Kwamba zaidi ya watu milioni 1.2 waliweza kufikiwa na kupata huduma za dawa za kufubaza makali ya virusi vya ukimwi, zaidi ya watu milioni 8.2 wamepata huduma na kupona Malaria, neti milioni 4 zimegawiwa bure nchi nzima, zaidi ya watu elfu 84 wamepona Kifua Kikuu na zaidi ya watu 391 wenye Kifua Kikuu sugu wapo kwenye matibabu.

“Kiwango cha VVU hapa Tanzania pia kimeshuka kutoka xxx mwaka mpaka xx mwaka 2016,” amesema Dkt. Bujari.

Amebeinisha kuwa kidunia Mkutano Mkuu wa uchangiaji wa Mfuko kwa Awamu ya saba utafanyika nchini Marekani kuanzia Septemba 19 hadi 21 mwaka huu kwamba fedha hizo zinategemewa kuokoa maisha ya wanadamu zaidi ya milioni 20 duniani kote ifikapo mwaka 2026.

WADAU WAZUNGUMZIA HALI YA DEMOKRASIA NCHINI

Mwenyekiti wa Chama Cha Wananchi (CUF) Prof. Ibrahim Lipumba akichangia katika mjadala, amesema kwamba hali ya Demokrasia nchini imekuwa ikisuasua katika kipindi cha miaka sita iliyopita.

“Tume ya Jaji Nyalali ilipendekeza kuandika Katiba Mpya na kufanya mabadiliko ya Sheria 40. Kuliendelea mbele bila kuwa na msingi mzuri wa kikatiba na sheria,” ameeleza Prof. Lipumba.

Mbunge wa Ubungo (CCM) Profesa Kitila Mkumbo amesema, ili wananchi washiriki vizuri katika Demokrasia ni lazima miiba iondolewe.

“Ni vizuri iandikwe Katiba ambayo itaongeza ushiriki wa wananchi katika Demokrasia. Katiba ikiendelea namna hii, mtaendelea kulia kila mwaka,” amesema Prof. Mkumbo.

Naibu Katibu Mkuu Bara wa ACT-Wazalendo Joram Bashange amesema “Tunahitaji kuwekeza kwa wananchi kwenye elimu ya Uraia,”. Ameeleza kuwa kama ACT-Wazalendo wametoa mapendekezo yao kwenye kikosi kazi kwamba ubadilishwe mfumo wa uchaguzi.

“Tutoke kwenye first past the post, twende kwenye proportional representation. Hii itaongeza ushiriki wa wananchi katika Demokrasia,” amesema.

Kwa upande wake Mbunge wa Viti Maalum (CCM) Neema Rugangira amesema kuwa ni vizuri kukawa na utaratibu wa kutenga nafasi Fulani za majimbo kwa ajili ya wanawake kwamba hiyo itavifanya vyama kuwajengea uwezo wanawake. 

No comments